Timu ya Namungo FC imepata kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Dodoma Jiji katika mchezo wa Ligi Kuu ya NBC #NBCPremierLeague uliochezwa leo kwenye Dimba la Ilulu mkoani Lindi.
Magoli ya Dodoma Jiji yamefungwa na Anuary Jabir na Emmanuel Martin wakati goli la Namungo likipachikwa na Bigirimana Blaise.